Archive for August 11, 2007

Msaada jamani!!

Leo hii, asubuhi sana na mapema nilipoingia ofisini kwangu, jambo la kwanza kabisa kulifanya ilikuwa kusoma barua nilizotumiwa na wasgirika mbalimbali kama ilivyo kawaida yangu. Moja kati ya ujumbe ambao nilikutana nao ni huu hapa chini kumhusu binti aliyeko pichani, ambao nitauweka kama ambavyo niliukuta.

 

===

Ukimuona kwa sura, ni msichana mzuri mwenye macho ya kuvutia, lakini masikini hana raha ya maisha! Mtoto Sofia James Mwiga (17, pichani)mkazi wa Manispaa ya Tabora nchini Tanzania anaishi kwa mateso kufuatia ugonjwa wa ajabu wa kuvimba miguu hali iliyomfanya ajione mpweke machoni mwa jamii huku akishindwa kuanza shule.


Licha ya baba yake kumtafutia matibabu kwa zaidi ya miaka 10 bado hajafanikiwa kwani kila Daktari anayemfanyia uchunguzi hutoa maelezo kuwa hapa Tanzania hawezi kufanyiwa oparesheni isipo kuwa nje ya nchi ambako kuna Wataalam na vyombo vya kitabibu vya kisasa.

Kutokana na umasikini alionao baba mtu ameshindwa kumsaidia badala yake amebaki akisubiri miujiza ya mungu ishuke pengine atapata mfadhili atakaye weza kumsaidia kupata matibabu hivyo anawaomba wasamaria wema popote duniani waweze kumsaidia kuokoa maisha ya mtoto wake huyo.


Hivi sasa mtoto huyu yupo katika hospitali ya Lugalo, jijini Dar es salaam akisubiri atakayeweza kujitokeza na kumsadia kupata matibabu sahihi nje ya nchi, kwa mujibu wa mdaktari, anahitaji operation ya kuondoa nyama hizo zilizozidi.

cheki anavyoumia

Mungu kama amekupa, basi kumbuka na wenye shida. Naamini kunamtu hapo anaweza kubadili masiha ya msichana huyu kwa uwezo wake mola! namba ya simu ya baba mzazi wa msichana huyu ni +255 753 916690.

Akiwa na jamaa

Nilipomaliza kuusoma ujumbe huo niliwasiliana na mwenye namba hiyo ambaye alijitambulisha kwa jina la Francis Aloyce Mwiga, ambaye ni baba wa wa binti huyo na akanieleza kuwa tatizo hilo lilimuanza mwaka 1998, lakini halikuwa kubwa sana, hadi mwaka 2005 ndipo hali ilipofumuka ghafla na hadi kufikia hali aliyo nayo binti huyo kwa sasa.

Alinipa ruhusa ya kupandisha ujumbe huu katika blogi yangu na ruhusa kwa yeyote atakayeupata kujitahidi kwa kadiri awezavyo kusambaza kwa watu wengine ili binti huyu ambaye ni dada yetu na rasilimali muhimu kwa Taifa la Tanzania, aweze kusaidiwa.

KUTOA NI MOYO JAMANI. MWENYE NACHO HAKIKA NI VYEMA AKASAIDIA WASIO NACHO. MSAADA WENU UNAHITAJIKA KUSAIDIA MAISHA YA BINTI YETU HUYU.

August 11, 2007 at 10:52 am 2 comments


Blog Stats

  • 35,839 hits
August 2007
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031