Archive for May 31, 2007

Taifa Stars, uchaguzi CCM & Uchaguzi wetu.

Kwa kweli najivunia Utanzania wangu, najivunia kuwa Mtanzania na ni mmoja kati ya tunaoombea ifikapo Juni 02, 2007, katika uwanja wa CCM Kirumba kule Mwanza, Mungu awe upande wetu ili maajabu yatokee kwa timu yetu ya taifa (Taifa Stars A.K.A JK Boyz), iliyowahi kuitwa kichwa cha mwendawazimu, kuwachinga Simba wa Teranga (Timu ya taifa ya Senegali). Inshaalah, kama wao wameweza kwanini sisi tushindwe bwana!! Ebo, wakitushinda uwanjani basi hata kwa mdomo pia!!

Kwa wale wanaofuatilia masuala ya kisiasa humu nchini mwetu, iwe ukiwa humu humu ndani, au ukiwa uko ughaibini, naamini kuwa kwa kipindi cha wiki kadhaa sasa, wamekuwa wakikutana na habari za Vigogo mbalimbali kutoka hiki chama kilichoshikilia kila kilicho kitamu nchini Tanzania (huku pia kikijitahidi kunyakua na zile chache , kama zipo, zilizobakia kwa wengine), kuumana makoo katika kuwania ulaji zaidi kupitia chama chao hicho. Habari za fulani kaibukia mkoa fulani, huyu kachukua huku, yule naye kafufukia NEC, sijui fulani kazindukia ujumbe wa CCM nk, ndizo ambazo nimekuwa nikikutana nazo katika kipindi hiki. Ah!! bwana wee, si tunaambiwa “majina makubwa yanamaanisha habari kubwa?”

Nyie ambao vichanga vyenu vunatupiwa mochwari vikiwa bado hai, nyie mnaolalamikia kuhujumiwa matokeo ya mitihani na akina kalagabaho wengine, kwakweli mlie tu. Kwa sasa nyie kurasa zenu zimefunikwa kwa muda katika tuvyombo twetu twa habari hapa nyumbani. Anyway, hali ndivyo ilivyo mwanawane, tuendelee kukandamiza maumivu yetu ndani yetu tukisubiri habari za wakubwa kuwania ulaji mkubwa zipite kwanza.

Tuyaache hayo, eeeh ni hivi; mwanane, nimejitokeza kugombea likiti la uenyekiti katika lijuiya letu la wana blogi, nawania linafasi la uenyekiti mwanawame kwahiyo naomba wajameni mnikandamizie mikura yenu ya kutosha tu, kusudi niweze kuliongoza lijumuiya hili changa. Kimsingi hakutakuwa na masufuria ya wali, wala sitawarestisha in pisi wanyama wa watu ili niwaandalie mapilau, lakini nadhani mtanikandamizia tu bila wasiwasi.

Lakini mwanawane, ukitaka kupata mitaarifa ya kutosha kuhusu lijumuiya letu lilikotoka, malengo na lilipo kwa sasa, unaweza tu kujimuvuzisha mwenyewe kwa kulitembelea liblogi la jumuiya kwa kukong’oli hapa, kisha mwenyewe utakuwa umeingia huko mwanawani ujionee mwenyewe lijuiya linavyozidi kuserereka kwa kwenda mbele. Halkafu mwanawame, ufuatilie limuchakato la uchaguzi wa hili lichama linalotawala nchini mwetu na ule wa lijumuiya letu.

Waveja mwanawani, neksti wiki lile lihabari la akili kumkichwa litakujia sehemu ya pili yake na ya mwisho kabisa.

May 31, 2007 at 11:44 am Leave a comment


Blog Stats

  • 35,835 hits
May 2007
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031