Archive for February, 2008
Kichwa cha ajabu duniani
Unamjua mtu mwenye kumbukumbu za ajabu sana humu duniani? Mtu ambaye unaweza kumtajia tarehe fulani miaka kumi iliyopita na kisha baada ya sekunde tano akaanza kuielezea siku hiyo kuwa ilikuwa siku gani, ilianza vipi, alifanya nini na nini cha muhimu kilitokea siku hiyo?
Wanasayansi nchini Marekani wameanza kufanya uchunguzi wa kina juu ya uwezo wa kiakili/kumbukumbu wa raia mmoja wa nchi hiyo ambaye inasemekana kuwa ndiye binadamu mwenye uwezo wa ajabu wa kuwa na kumbukumbu kichwani mwake. Soma zaidi habari hii kwa kubonyeza hapa..
2 comments February 24, 2008
Kilichomng’oa Lowasa madarakani
kwa marefu na mapana, naomba wasomaji wangu mpate fursa ya kupitia kitu kipya leo ambacho loicha ya kuwa si picha, lakini kimeleta picha mpya katika historia ya taifa la Tanzania. Namaanisha ripoti kuhusu kashfa ya Kampuni hewa ya kuzalisha Umeme iitwayo Richmond. Ripoti hiyo iliwasilishwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katikati ya wiki linaloelekea ukingoni, na kusababisha kishindo kikubwa sana katika medani za siasa za Tanzania.
Najua si wote mliiona ripoti hiyo ilipokuwa ikiwasilishwa Bungeni, na si wote mliosikia, na pia si wote mmeweza kuipata. Sasa kwa wale ambao hawakubahatika kote huko, naomba muipitie kwa kubonyeza hapa.
Add comment February 9, 2008
