Una ushahidi wa yanayojiri Kenya?

January 10, 2008

Ni hulka ya binadamu, kujifunza kupitia makosa. na hili ndilo linalojitokeza nchi jirani na hapa kwetu TZ.

Wakati ambapo hakuna mtu ambaye alidhania kuwa yanayojiri nchini Kenya hivi sasa yangetokea, na wakati kila mtu akiwa anasikitika kutokana na hayo yanayoendelea huko, kwa upande wa pili, wanablogu wa nchini humo wameonyesha mchango wao mkubwa sana katika kuona hali inabadilika.

 Jitihada za mwanzo kabisa zilikuwa zile za kuhakikisha kuwa dunia inatambua kilicho, kinacho na hata kitakachotokea nchini mwao, kwa kutusambazia habari na matukio mbalimbali kwa kadiri walivyoweza. jitihada ya karibuni kabisa imekuwa ni kuanzishwa kwa zana inayoitwa Ushahidi.

Kwa sasa pengine sitokuwa na mengi sana kuihusu zana hii, maana nami niliipitia juu juu tu baada ya kupata taarifa hizi kupitia kwa kaka yangu Ndesanjo wa Jikomboe. ambaye naye aliipata kupitia kwa Mwafrika Mweupe….nitawaomba tu muitembelee na muone mambo yanayoendelea huko.

Na wakati mkifanya hivyo, ni vyema tukakumbushana umuhimu wa kuungana na kuzidi kuiombea heri nchi ya Kenya.

Entry Filed under: maskani. .

1 Comment Add your own

Leave a Comment

Required

Required, hidden

Some HTML allowed:
<a href="" title=""> <abbr title=""> <acronym title=""> <b> <blockquote cite=""> <cite> <code> <pre> <del datetime=""> <em> <i> <q cite=""> <strike> <strong>

Trackback this post  |  Subscribe to the comments via RSS Feed


Bango la Matangazo & Wazo mahususi

Blogi Nyingine

Blogi za Katuni

Blogi za Picha

Malavidavi!

Mapishi

Mavazi & Mitindo

Vyombo vya Habari

wageni

Webu mseto

Blog Stats

 

January 2008
M T W T F S S
« Dec   Feb »
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  

Archives

Meta

Pages