Archive for November 7th, 2007
Waraka wa Butiku kwa Mkapa huu hapa
“Mali imeanza kuchukua nafasi ya uzalendo na kutumiwa na viongozi wengi wa CCM kama nyenzo ya uongozi bora wa kisasa. CCM imeanza hata kutoona haya, na viongozi wakuu, chini ya uongozi wako sasa wamenyamaza, wanaona haya kukemea uovu” – Hiyo ni sehemu ya maneno yaliyoko katika waraka wa Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku, aliomuandikia mwenyekiti mstaafu wa CCM, taifa, Benjamin William Mkapa.
Inawezekana kweli kuwa mzee Butiku, akiwa kama mmoja wa viongozi wa ngazi mbalimbali za juu za kiserikali na chama enzi zake, hakufanya jambo lolote la maana kuhakikisha hali haifikii katika kiwango tunachokisoma katika waraka huu, kama alivyosema mchangiaji mmoja kule kwa kaka yangu Jeff wa harakati, lakini sidhani kama hicho kinaweza kuwa kigezo cha kukosoa haya anayosema kwasababu yana mantiki ndani yake na hali ndivyo ilivyo.
Soma waraka huo ambao wiki kadhaa zilizopita ulizua majibizano baina yake na viongozi kadhaa walioko madarakani hivi sasa. Bonyeza hapa kuusoma.
1 comment November 7, 2007
