Jamani nimeshindwa mnisamehe
September 8, 2007
Wakati natoa tangazo la kuhamisha kijiwe hiki toka kule blogspot, nilitangaza pia kuwa nimeanzisha kijiwe cha picha kupitia hukuhuku wordpress. naomba niseme kuwa nimechemka kupandisha picha katika wordpress.
Kutokana na hali hiyo basi, kijiwe cha picha mbalimbali nitakazokuwa nazipata huko mitaani ninakokatiza zitakuwa zikipatikana kupitia http://www.nilichokiona.blogspot.com/
Tayari kuna matukio kadhaa huko ambayo si busara ukiyakosa. Unajua ilikuwaje mpiganaji Mbowe alipotembelea jiji la Mbeya? Unajua kuwa basi la Sabco limechinja tena watu 27, ikiwa ni chini ya miezi miwili toka lichinje tena watu 12 mkoani Mbeya?
Tembelea kijiwe changu cha picha uyaone haya live. Bonyeza hapa.
Entry Filed under: Uncategorized. .

Trackback this post | Subscribe to the comments via RSS Feed