Archive for August 24th, 2007
Msanii wa Bongo Fleva ndani ya Blogu
Wengi wetu tulitarajia na tulijua kuwa ni suala la muda tu, tungeweza kumwona Freddy Macha mtandaoni, lakini ni nani alitarajia ujio wa Ilunga Khalifa? Eh!! Kuna watu tayari wanajiuliza naye ni nani.
Huyu jamaa ambaye anaringia simu yake ya kamera (sijui ni nzuri kama hii yangu au vipi), kwa jina anaitwa Ilunga Khalifa. ukipenda unaweza kumuita CP au Cpwaa kama vijana wanavyopenda kumwita huko mitaani na ujio wake kwakweli umenisisimua sana. Msanii kwenye Blogu!! Inashangaza eeh!!
Sasa ngoja nikwambie kitu… Ilunga Khalifa, ni mmoja kati ya wasanii kadhaa wa huu muziki wa kizazi kipya, ambao wamefanikiwa ‘kuwashika’ vijana vilivyo kutokana na nyimbo zao zenye mistari ya aina yake.
Si mpenzi sana wa aina hii ya muziki, lakini nilishawishika kusikiliza muziki wake mmoja, baada ya kuiona blogi yake na kuambiwa kuwa ni msanii. Kwa wale vijana wanaoufuatilia sana muziki huu, naamini wanaujua wimbo wake uliowakamata vilivyo, unaokwenda kwa jina la CPwaaa.
Wakati wasanii wetu wengi hapa nchini wakiwa wanafanya kazi zao katika hali ambayo hata sisi tumekuwa tukiilalamikia kila siku, bilashaka kutokana na elimu ndogo waliyonayo wengi wao, huenda Khalifa, akawa kawafungulia milango wenzake kwa ajili ya kuweza kuchangamana na dunia inayowazunguka.
Sijui kama wenyewe wanaweza kunielewa kwakweli, ila naamini kwa wale wenzangu na mie ambao tumeshaogelea huku, naamini mnanielewa namaanisha nini.
Nitazungtumza zaidi kuhusu msanii huyu pindi nikishapata wasaa nikakutana naye na kuzungumza naye mawili matatu. Kwa leo, naomba niwape mwito wa kumtembelea CP, na kisha kumpa mawili matatu katika kijiwe chake. Pia muweze kushuhudia kile anachokiona kupitia kamera yake ya kwenye simu.Bonyeza hapa kumtembelea na kumkaribisha
Add comment August 24, 2007
