Archive for March 18th, 2007
Natafuta funguo
Wapendwa wasomaji, marafiki, wakosoaji na wale wote ambao mmekuwa mkinitembelea kijiweni kwangu kwa muda wote toka nianzishe kijiwe hiki, napenda kuwaomba radhi kwa kuwa kimya kwa muda mrefu kiasi sasa. nakiri kuwa nimekuwa nikikawia sana kuwaletea gumzo jipya mara kwa mara kama ilivyiokuwa awali, lakini mnisamehe sana maana kwakweli nimebanwa na masomo kwa wakati huu. Na kama mnavyojua wahenga walihanikiza “Elimu ni Ufunguo wa Maisha” kwahiyo nimetingwa kidogo na shughuli ya kusaka ufunguo wa maisha yangu.
Nawashukuru sana kwa kuniunga mkono, na nawaahidi kuwa niko pamoja nanyi daima, na pindi masomo yakipungua ukali kidogo, nitajitahidi sana kuwaletea yale mapya niliyokumbana nayo katika safari hii ya sasa.
2 comments March 18, 2007

