Eti nchini Libya unaweza kumpinga Mungu ila si Gaddafi

October 28, 2006

Habari hii nayo niliikuta katika jumba la Macha, na ikanivutia sana tu kwasababu inanigusa kwa kila hali. Ni kuhusiana na Uhuru wa Vyombo vya Habari. Kwa mujibu wa masimamo wa “ligi” ya Uhuru wa vyombo vya Habari, Duniani, uliotolewa na Shirika la Wana-Habari wasio na mipaka, Tanzania ni nchi ya 88, ikiwa imezidiwa hata na Liberia, ambayo ni ya 84 (Macha, naomba urekebishe kidogo hapo).

Nchi zilizoshika nafasi tatu za juu ni Finland, Iceland na Ireland, huku nchi za tatu kutoka chini zikiwa ni Korea Kaskazini, Turkmenistan na Eritrea. Maswali ambayo yalitumika katika kuandaa ripoti hiyo yalikuwa haya, na upangiliaji wa ripoti yenyewe baada ya kukusanywa kwa majibu ya maswali hayo ulikuwa huu hapa.

Lakini pengine sehemu ambayo sisi wanahabari wote kwa ujumla wetu, mahali na wakati wowote ule tunatakiwa kupawekea mtizamo wa kipekee, ni kwenye taarifa za yanayoendelea nchini Libya, ambako inadaiwa eti ni aheri kumpinga Mungu ukiwa mwanahabari huko, kuliko kumwandika vibaya rais wa nchi hiyo, yaani komredi Muammar Gaddafi

Entry Filed under: maskani. .

1 Comment Add your own

  • 1. James  |  October 30, 2006 at 11:04 am

    Msangi, sijakuelewa…… Gaddafi huyu huyu ambaye kwa sasa anaonekana kama kinara wa kuiunganisha Afrika? Habari hii imenisisimua sana kwakweli

Leave a Comment

Required

Required, hidden

Some HTML allowed:
<a href="" title=""> <abbr title=""> <acronym title=""> <b> <blockquote cite=""> <cite> <code> <pre> <del datetime=""> <em> <i> <q cite=""> <strike> <strong>

Trackback this post  |  Subscribe to the comments via RSS Feed


Bango la Matangazo & Wazo mahususi

Blogi Nyingine

Blogi za Katuni

Blogi za Picha

Malavidavi!

Mapishi

Mavazi & Mitindo

Vyombo vya Habari

wageni

Webu mseto

Blog Stats

 

October 2006
M T W T F S S
« Sep   Nov »
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031  

Archives

Meta

Pages